Ndugu Watanzania/Americans,
Kwa niaba ya mwenyekiti wa jumuiya ya watanzania WA, ninawaandikia kuwa, uongozi wa TANZA-SEATTLE, unaomba kukutana na Watanzania (Bara na Visiwani) wote wa maeneo ya Bellevue, Kirkland, Renton, na vitongoji jirani.
Lengo la mkutano huu:
1) Kuhamasisha watanzania/Americans na rafiki wengine kujiunga na TANZA-SEATTLE- registration form zitakuwepo
2) Kupokea maswali/ maoni namna gani jumuiya iendeshwe
3) Kuhamasisha watanzania wachukue fomu za kugombea uongozi- uchaguzi ni Mwezi Januari: Fomu zitakuwepo
4)Kuhamasisha watanzania wahudhuria kwenye Annual Meeting ya Tanza-Seattle hapo January
Mahali pa kukutana: 411 156th Ave NE,Bellevue WA 98007
Muda: Saa nane (2:00pm) Mchana, mpaka saa kumi (4:00pm) jioni
Tarehe: Jmosi tar. 31 December, 2011
Tunaomba watu wote mjitokeze. Ninatambua kuwa sina email za watu wote, hivyo kama utapata ujumbe huu tafadhali mjulishe na mwenzio.
Kedmon Mapana
Katibu
No comments:
Post a Comment