Wanachama wa CCM tawi la DMV tunaungana na watanzania wenzetu popote duniani kutoa salamu Za rambi rambi kwa wanachama wa chama cha chadema kwa kuondokewa na kiongozi wao mheshimiwa Bob Makani.
Mheshimiwa, Bob Makani atakumbukwa kwa hoja zake za kuchangia mambo mbali mbali yaliyoweza kulijenga taifa la Tanzania. Wanachama wa chadema wameondokewa na kiongozi imara katika safu za vyama vya upinzani.
Sisi wanancham wa CCM tawi la Washington, DC Maryland na Virginia tunatoa salamu za rambi rambi kwa ndugu wa marehemu na wanachama wa chadema popote duniani.
Poleni sana
Katibu wa CCM
Tawi la CCM-DMV
Yacob Kinyemi
Marekani

No comments:
Post a Comment