Monday, May 20, 2013

MKUTANO MAALIMU WA KIROHO KUFANYIKA HOUSTON TX


Mwenyekiti wa jumuia ya watanzania wasabato walioko Marekani iitwayo Tanzania Adventists in the United States (TAUS), Bwana Jeoffrey Ngullu, amewatangazia watanzania wote kwamba mkutano mkuu wa kiroho kwa mwaka umekaribia. Bwana Ngullu, aishie Philadephia, jimbo la Pennsylvania, amesema kufuatia kufana kwa mkutano wa mwaka jana ulifanyika Washington D.C, uongozi wa TAUS umeamua mkutano wa mwaka huu (TAUS Retreat 2013) ufanyike Houston TX. TAUS inawaalika wote kujumuika, kufahamiana na kujifunza pamoja.

TAREHE ZA MKUTANO: Julai 11-14, 2013

MAHALI- Oak SDA School, 11735 Grant Road, HOUSTON, TEXAS 77429 USA

MGENI RASMI: Mchungaji Lucas Nzungu wa Arusha University, Tanzania

Gharama za mkutano ufikapo TX- ikiwemo chakula, usafiri na hoteli (Holiday Inn)- ni $292.50 kwa mtu aliye tayari ku’share’ chumba (double bed). Kwa wanaotaka chumba cha pekee jumla yao ni $465. Kuna wafadhili kadhaa TX wanaoweza kusaidia gharama za malazi, usafiri na chakula ufikapo Houston. Tafadhali wafahamishe mapema kama utahitaji ufadhili huo.

Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na mmoja wa wafuatao- Msafiri Lugoe (TX) 281-760-6805; Jeoffrey Ngullu (PA) 267-582-6276; au Shukrani Magoma (DC) 202-607-1976. Asanteni sana na mnakaribibishwa.

No comments: