ANGALIA LIVE NEWS

Friday, November 15, 2013

HUU NI USHINDI KWA AFRIKA, HATARUDI NYUMA-BALOZI MACHARIA

Mwakilishi wa kudumu wa Kenya kwenye Umoja wa Mataifa balozi Macharia Kamau amesema kile kinachoonekana kama kushindwa kwa ombi la Umoja wa Afrika kwenye baraza la usalama la Umoja wa Mataifa la kutaka kusitishwa kwa uchunguzi na mashtaka dhidi ya viongozi wa Kenya
yaliyoko Mahakama ya kimataifa ya Uhalifu, ICC ni ushindi mkubwa kwa Afrika.

Katika maohjiano maalum na Joseph Msami wa idhaa ya Kiswahili ya radio ya Umoja wa Mataifa muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao cha baraza la usalama, balozi Macharia amesema Umoja wa Afrika haujakata tamaa na kwamba wana uhakika wa ushindi dhidi ya ombi lao watakaolipeleka kwenye mkitano maalum the Hague Uholanzi wiki ijayo. Akifafanua kwa msisimko hisia zake kuhusu maamuzi ya baraza la usalama balozi Kamu anaanza kwa kushangaa wanaosema Afrika imeshindwa.

(SAUTI –MAHOJIANO MACHARIA)
Kusikiliza mahojiano bonyeza hapa

No comments: