Sunday, November 24, 2013

KINANA AWASILI SALAMA KYELA

Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana akishuka kwenye meli ya MV.Songea cha Liuli na kuwasalimu wananchi kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea Kyela akitokea Wilaya ya Nyasa  mkoani Ruvuma.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kijiji cha Mkini wakati wa safari yake kwa kutumia ziwa Nyasa kuelekea Kyela
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu ABdulrahman Kinana akicheza ngoma ya  Mganda akishirikiana na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro ,Katibu Wa NEC Itikadi na  Uenezi Nape Nnauye.
Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa akihutubia wakazi wa kijiji cha Mkini kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea Kyela.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongea na muzaji wa samaki pamoja na mihogo ya kuchemsha kwenye bandari ya Lupingu mnamo saa saba na nusu ya usiku katikati ni Dk.Asha-Rose Migiro.
Nahodha Mkuu wa Meli ya MV Songea  Ndugu Thomas Samuel Faya akitoa maelekezo namna ya kuiongoza meli kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro pamoja na Katibu wa NEC Itikadi  na Uenezi Nape Nnauye.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishuka toka kwenye meli baada ya kuwasili salama kwenye bandari ya Kyela na kupokelewa na viongozi mbali mbali wa Siasa na Serikali.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa kwa furaha na wakazi wa Kyela.
Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro akiwasalimu wakazi wa Kyela waliojitokeza kuja kuwapokea.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa na viongozi wa Chama na Serikali kwenye bandari ya Itungi ambayo muda si mrefu  itatengenezwa na kuanza kutumika.

No comments: