ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, March 16, 2014

ADEN RAGE: SIGOMBEI TENA UONGOZI SIMBA – UCHAGUZI MKUU MEI 4 MWAKA HUU!!


20140316-133233.jpg
MWENYEKITI wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage, jana ametangaza rasmi kwamba hatagombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo unaotarajiwa kufanyika Mei 4 mwaka huu.
Hata hivyo Rage kabla ya kutangaza maamuzi yake ya kutotetea cheo hicho katika uchaguzi mkuu ujao, wanachama wa klabu hiyo walianzisha vurugu katika mkutano mkuu huo uliotishwa maalumu kwa ajili ya kufanya marekebisho wa katiba kutokana na kiongozi wao huyo kuwaita ‘mbumbumbu’.
Kufuatia kauli hiyo, Rage, alilazimika kuwaomba radhi wanachama hao zaidi ya 571 waliohudhuria mkutano huyo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Bwalo la Polisi, Oysterbay jijini Dar es Salaam.

“Napenda kuwaomba radhi wanachama wenzangu kutokana na nilivyosema tuache umbumbumbu, lakini sikuwa namaanisha kama wengi wenu mlivyoelewa,” alisema Rage.
Licha ya kusema hatagombea tena uongozi, Rage, alisema ataendelea kuwa mwanachama mwaminifu wa Simba na atatoa mchango wake ili kufanikisha maendeleo.
“Nitatoa mchango wangu wa hali na mali, sina ugomvi na mtu yoyote na bado nina mapenzi na Simba,” aliongeza.

No comments: