Leo
Tarehe 22/03/2014 katika Manispaa ya Dodoma, Umoja wa Vijana wa Chama
Cha Mapinduzi (UVCCM), tumezindua mbio maalum za pikipiki zenye lengo la
kuhamasisha uzalendo miongoni mwa vijana na kuibua fursa zinazopatikana
maeneo mbalimbali ya Tanzania.
Mbio
hizi maalum zimezinduliwa na Rais waAZanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Zanzibar na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Mheshimiwa Dr.
Ali Mohamed Shein, katika hafla fupi ya kufana iliyofanyika katika makao
makuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa Dodoma.
Mbio
maalum za pikipiki zitazunguka nchi nzima na zitahitimishwa rasmi kwa
matembezi ya miguu kuanzia Kibaha Mkoani Pwani hadi Dar es Salaam tarehe
25/04/2014 yatakayopokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Mrisho kikwete katika ukumbi wa Nyerere
Convention.
Kauli Mbiu Yetu
"MIAKA 50 YA MUUNGANO; VIJANA TUDUMISHE MUUNGANO WETU NA TUTUMIE FURSA ZILIZOPO KULETA MAENDELEO YETU"
TANZANIA KWANZA, MENGINE BAADAYE
Imetolewa na;
Paul C. Makonda
Katibu wa Hamasa uhamasishaji UVCCM

No comments:
Post a Comment