ANGALIA LIVE NEWS

Friday, April 18, 2014

Kesho UKAWA watafanya mkutano wa hadhara Zanzibar

Kesho, Jumamosi Aprili 19, 2014 Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wamepanga kufanya mkutano wa hadhara Zanzibar kwa malengo ya kuongea na wananchi juu ya msimano wao wa kususia vikao vya Bunge.
Akizungumza jana na waandishi wa habari mjini Dodoma, mwakilishi wa kundi hilo Profesa Ibrahim Lipumba alisema kuwa katika kikao chao wamekubaliana kuzunguka nchi nzima kufanya mikutano ya hadhara kwa
wananchi kwa kuwajumuisha wajumbe wasiokuwa na dharura.
“Tumekubaliana kwamba siku ya Jumamosi kwa
pamoja Wabunge wote ambao hatuna dharura tukuwa tumeenda Zanzibar, kutakuwa na mkutano wa hadhara kuanzia saa nne asubuhi. Tutaondoka na siku hiyo na Boti ya saa moja asubuhi kuelekea Zanzibar. Katika mkutano wa Zanzibar tutaeleza yaliyojiri katika Bunge hili Maalumu....” alisema Lipumba kama anavyosikika kwenye video iliyopachikwa hapo chini.
Viongozi wa Ukawa walotoka nje ya Bunge Maalum jana wakipinga jinsi mjadala wa Katiba Mpya unavyokwenda, na kudai kuwa hawako tayari kurudi Bungeni humo wiki ijayo, wala hawatarejea kwenye kikao cha Agosti, endapo hawatahakikishiwa kuwa maudhui yaliyomo ndani ya Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya yatajadiliwa kama yalivyo.

Mwenyekiti wa Bunge hilo, Mhe. Samuel Sitta amesema anawasihi Wajumbe hao warejee katika Kamati ya Uongozi ili waeleze hatima ya uamuzi wao kwa maana una athari kisheria na kiutawala.

No comments: