Advertisements

Wednesday, April 16, 2014

Mhifadhi mkuu apigwa risasi DRC


Sokwe hawa wa milimani wanakabiliwa na tisho la kutoweka kutokana na kuwindwa sana
Mmoja wa viongozi wakuu wa
uhifadhi wa wanyama pori barani Afrika Emmanuel de Merode, amejeruhiwa vibaya baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika moja ya mbuga kongwe barani afrika.
Bwana Merode,ambaye ni raia wa Ubelgiji ni mkurugenzi wa mbunga ya wanyama pori ya Virunga,ambayo ni makao ya Sokwe wanaokaa milimani katika Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Sokwe hao ni baadhi ya wanyama walio katika hatari ya kutoweka kutokana na kuwindwa sana.
Alipigwa risasi akiwa anaendesha gari kati ya eneo lililo kati ya makao makuu ya mbuga hiyo na mji wa Goma ambako amelazwa hospitalini.
Sababu ya kupigwa risasi kwa mhifadhi huyo haijajulikana, lakini makundi ya watu ambao hukata miti kiharamu, wawindaji haramu na waasi huendesha shughuli zao katika eneo hilo.

No comments: