Kaimu rais wa Ukraine Olexander
Turchynov amesema kuwa vikosi vya kijeshi vya Ukraine vimeuteka na
kuuthibiti uwanja mmoja wa kijeshi katika eneo la Kramatosk mashariki
mwa Ukraine,baada ya mapigano na
makundi yanayounga mkono Urusi.Rais huyo ameliambia bunge la taifa huko Kiev kuwa operesheni hiyo maalum inafanywa hatua kwa hatua .
Bwana Turchynov aliliambia bunge kuwa
operesheni ya kukomboa miji na mali ya umma kutoka mikononi mwa ''Mgaidi'' itaendelea kuambatana na sheria za kibiniadamu.
Mamia ya watu wanaodaiwa kuwa wanaharakati wanaounga mkono Urusi wamekongamana nje ya uwanja huo wakiwafokea majeshi waliotua humo kutoka Kiev.
Makundi ya waasi wanaounga mkono Urusi wameteka takriban miji 10 katika mashariki mwa taifa hilo .
Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kuwa Ukraine huenda ikatumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe iwapo kiev itaendelea na operesheni hiyo dhidi ya wananchi wake waasi.
Taarifa kutoka Kremlin zinasema kuwa Putin alitoa tahadhari hiyo katika mazungumzo ya simu na Kiongozi wa Ujerumani bi Angela Merkel.
Viongozi hao wanasemekana kuafikiana kuhusiana na umuhimu wa mkutano wa kwanza wa pamoja baina ya Bara Ulaya Urusi Ukraine na Marekani.
Mkutano huo unatarajiwa kufanyika huko Geneva Uswisi.
Miji iliyoko Mashariki mwa ukraine zinataka kura ya maoni kufanyika huko kuamua iwapo wanataka kuendelea kuwa sehemu ya Ukraine ama wangependa kuiga mfano wa Crimea iliyoamua kujitenga na kujiunga na Urusi baada ya
utawala mpya kumng'oa madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo Victor Yanukovich .
bbc
No comments:
Post a Comment