Kamanda wa polisi Mkoa wa Geita Kamishina msaidizi wa polisi Joseph Konyo.
Siku
chache baada ya mkuu wa polisi wilaya ya Geita Mrakibu mwandamizi wa
polisi Sadock Busee Bwire kuangusha gari la polisi PT 1998 alilokuwa
analiendesha,na kuamriwa na Kamanda wa polisi Mkoa wa Geita Kamishina
msaidizi wa polisi Joseph Konyo alitengeneze kwa pesa zake kwa madai kuwa kwa cheo chake hatakiwi kuendesha gari la polisi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakuu wa vituo vya
Butundwe,Katoro,Mgusu,Nyarugusu,Kasamwa,Lwamgasa,Nyamboge,Nzera,na
Nyakagwe wamelalamikia hatua hiyo ya Ocd kuwaamuru kuchangia gharama za
matengenezo ya gari hilo
“huyu ocd wetu simuelewi anatuambia tuchangie hela sisi tunapata wapi?au
ndio kusema anatuagiza tuwaonee wananchi ili tupate hela ya kumpa?
Alihoji mmoja wa wakuu wa vituo
Awali akizungumzia ajali hiyo Kamanda Konyo alisema Ajali hiyo ilitokea
Mei 7 mwaka huu usiku saa 2 katika kijiji cha Bufunda tarafa ya Busanda
ikiwa imebeba watuhumiwa wa makosa mbalimbali huku
baadhi ya watuhumiwa wakitoroka,chanzo cha ajali hiyo licha ya kufichwa
imeelezwa kuwa ni mwendo kasi wa dereva wa gari hiyo.
Aliwataja watuhumiwa waliotoroka kuwa ni William Michael,Charles
Julius,Mussa Mashiri,Joseph John,Nelson Raphael,na Sued Omary wote
wakazi wa Nyarugusu.
Aidha Kamanda Konyo alisema kuwa kwa mujibu wa kanuni na sheria za
polisi “Police General Order” mkuu wa polisi wa wilaya ana dereva wake
haruhusiwi kuendesha gari la polisi isipokuwa la kwake binafsi.
Aliongeza kuwa askari mmoja kati ya watatu aliyejulikana kwa jina la
Konstebo Linus wa kituo cha polisi Nyarugusu alijeruhiwa baada ya meno
yake mawili kung’oka na kulazwa katika hospitali ya wilaya kwa matibabu.
Kaimu mganga mkuu wa hospitali ya wilaya Dk.Adam Sijaona alikiri kulazwa kwa askari huyo na kudai hali yake inaendelea vizuri.
Aidha askari polisi wa kituo kikuu cha Geita wamekuwa wakimtuhumu mkuu
wa polisi huyo wa wilaya kwa madai kuwa anashirikiana na wafanyabiashara
wa magendo hasa wa mkaa,na pombe kali aina ya viroba zinazoingizwa
kinyume nchini kutoka nchini Uganda.
Wamedai kuwa baada ya kuwakamata wafanyabiashara hao ambao ni maswahiba
wa Ocd wakisafirisha magendo na kuwafikisha mahakamani,Ocd huyo ameamua
kuwachongea uhamisho na kupelekwa wilaya za Nyang’wale Chato na
Mbogwe,uhamisho ambao wameuita ni wa fitina wala sio wa haki.
Wameeleza kuwa licha ya gari ya polisi kuangushwa na kuharibiwa hakuna
jalada lililofunguliwa kituoni hapo na haikukaguliwa na mkaguzi wa
magari kama taratibu zinavyoelekeza na badala yake ilifichwa kwenye
gereji bubu ili kuficha ukweli,hali ambayo imezua hofu kwa askari
aliyeumia kuwa atakosa haki zake .
Jitihada za kumpata mkuu wa polisi wa wilaya Sadock Busse Bwire kujibu
tuhuma zinazomkabili hazikuzaa matunda,baada ya simu yake kuita kwa
muda mrefu bila kupokelewa,na alipotumiwa ujumbe wa maneno hakujibu.
Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Kamishina
msaidizi wa polisi Joseph Konyo alipoulizwa hatua ya wakuu wa vituo
kuamriwa kuchangia gharama za matengenezo ya gari hiyo,alidai
hawalazimishwi na wala hakuna sheria inayowabana wasipochangia,alidai kuwa analifuatilia suala hilo na baada ya hapo atalitolea ufafanuzi.
Na Valence Robert wa Malunde1 Blog- Geita
No comments:
Post a Comment