ANGALIA LIVE NEWS

Saturday, June 28, 2014

TRAFIKI WATAKIWA KUACHA KUJIFICHA VICHAKANI


Serikali imewataka askari wa USalama BArabarani, maarufu kama Trafiki, kuacha mara moja tabia ya kujificha vichakani na kujitokeza ghafla kusimamisha magari yanayokwenda mwendo kasi.
Kauli hiyo ilitolewa Bungeni jana na
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima aalipokuwa akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Musoma Mjini Vincent Nyerere (CHADEMA).
Katika maelezo yake Silima alisema “kama lengo la askari ni kukaa katika vichaka kwa ajili ya kujikinga na jua kali hiyo ni sawa, ila si kusimamisha magari kwa mtindo huo. Sheria zipo wazi iwapo itathibitika kuwa askari wa usalama barabarani amesababisha ajali.”

2 comments:

Anonymous said...

Sioni tatizo trafic kujificha. Huo ni kawaida. Hata wenzetu US traffic wao anajificha kuna sa wahalifu.

Anonymous said...

nafikiri huu ni mtindo au mbinu wanazotumia maaskari kuwastukizia wavunja sharia. hata Marekani ni hivyo hivyo wanajificha msituni na camera zao hata magari yao ni ya rangi ya msitu. Madereva wafuate sharia na ndio solution.