ANGALIA LIVE NEWS

Wednesday, July 16, 2014

BALOZI MDOGO OMAR MJENGA AFANYA MKUTANO NA CHINESE CHAMBER OF COMMERCE OF DRAGON MART YA DUBAI

Chinese Chamber of Commerce of Dragon Mart, Dubai, wapo tayari kuja Tanzania na kuanza mazungumzo na Wizara ya Viwanda na Biashara, pamoja na TanTrade, kuhusu uwezekano wa kujenga uwanja wa kisasa wa maonyesho ya kimtaifa ulipo uwanja wa sasa wa Sabasaba wa Mwalimu Nyerere. Nia, nik kuwa na maonyesho hayo kwa kipindi cha mwaka mzima.


Bw. Jin Guozhong, amemhakikishia Mheshimiwa Balozi Mdogo kuwa, nia yao ni kujenga uwanja wa maonyesho hayo ili kuwa kama kituo kitakachohudumia nchi zote za jrani na Tanzania. Waliomba kupata taarifa za mazingira ya uwekezaji Tanznaia, na tumekubaliana kuwa watafanya ziara nchini Tanzania katikati ya mwezi Agosti ili kukutana na Waziri wa Viwanda na Biashara na wadau wengine wote.
Mheshimiwa Balozi Mdogo Omar Mjenga akifanya mazungumuzo Chinese Chamber of Commerce of Dragon Mart, Dubai ambao wamekubali kuwekeza nchini Tanzania.
Bw. Jin Guozhong, Mwenyekiti wa Chinese Chamber of Commerce of Dragon Mart, Dubai.akimsikiliza Mheshimiwa Balozi Mdogo, Omar Mjenga wakati walipokua wakifanya mazungumuzo na wao kukubali kuja kuwekeza nchini Tanzania.
 Kikao kikiendelea
Mheshimiwa Balozi Mdogo akiwa na wageni wake. Anayesalimiana naye ni Bw. Jin Guozhong, Mwenyekiti wa Chinese Chamber of Commerce of Dragon Mart, Dubai. Wengine ni washauri wake wa masuala ya uwekezaji.

No comments: