Advertisements

Thursday, July 24, 2014

TAARIFA KWA UMMA KUHUSIANA NA KIVUKO CHA MV. KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UJENZI
WAKALA WA UFUNDI NA UMEME (TEMESA)

   
Telegrams TEMESA DSM                                                             S.L.P  70704
Simu: +255-22-2862796/97                                                             DAR ES SALAAM
Fax:   +255-22-2865835                                                                  TANZANIA



TAARIFA KWA UMMA

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) anawatangazia wananchi wote kuwa kivuko cha MV. Kigamboni kinatarajiwa kwenda kwenye matengenezo makubwa wakati wowote kuanzia leo.
Hivyo huduma za uvushaji zitaendelea kwa kutumia vivuko vya MV. Magogoni pamoja na MV. Lami katika kipindi chote cha matengenezo husika.
Uongozi wa TEMESA unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakao jitokeza.
Imetolewa na Ofisi ya Mtendaji Mkuu
TEMESA
          23/7/2014

No comments: