
Waziri wa elimu aliamuru zisifunguliwe ili kuwapa walimu mafunzo jinsi ya kushughulikia ugonjwa huo.
Huu ndio uzukaji mkubwa zaidi ambapo watu 2615 wanakadiria kuambukizwa na angalau nusu yao kuaga dunia.
Virusi hivi vinaenezwa kwa wanadamu kupitia maji maji ya mwili .
Takwimu za maambukizi ya Ebola
Ugonjwa huuu hauna tiba, ila kwa kuangaliwa vyema bila shaka mtu anaweza kuishi zaidi.
Ulienea Nigeria nchi iliyo na watu wengi zaidi mwezi Julai baada ya mtu aliyekuwa na virusi kutua nchini humo kutoka Liberia.
Serikali ya Nigeria inatarajia kukomesha kuenea zaidi kwa ugonjwa huu kwani sasa ni mtu mmoja tu aliye na ugonjwa huo wa ebola .
Waziri wa elimu Ibrahim Shekarau amesema Inatarajiwa angalau wafanyikazi wawili kila shule katika zile za umma na za kibinafsi watapata mafunzo maalum ya ugonjwa huu kufikia septemba 15 jinsi ya kupambana na visa vinavyoshukiwa kuwa vya Ebola
Shirika la Afya duniani WHO lilisemakuwa mlipuko huu wa ugonjwa wa Ebola imewaambukiza madaktari wengi sana.
WHO ilitoa taarifa ambayo ilionesha kuwa zaidi ya watu 2600 Guinea ,Liberia,Nigeria na Sierra Leone wameugua ugonjwa huu ulioanza mei pamoja na wafanyakazi wa huduma za afya 240.
Maambukizi kwa wafanyi kazi wa afya yanatokana na uhaba wa vifaa vya kujipinga na wafanyikazi kwani daktari mmoja anawahudumia wagonjwa 100,000 katika nchi zingine.
BBC
WHO ilisema kuendelea kwa madaktari kuambukizwa virusi kunapelekea juhudi za kuzuia ugonjwa huu kudidimia kwani hospitali zingine zimeanza kufungwa.
WHO ilisema kuendelea kwa madaktari kuambukizwa virusi kunapelekea juhudi za kuzuia ugonjwa huu kudidimia kwani hospitali zingine zimeanza kufungwa.
No comments:
Post a Comment