Advertisements

Wednesday, November 19, 2014

KONGAMANO LA VIJANA LA SIKU MOJA LAFANYIKA JIJINI DAR

Taasisi isiyo ya Kiserikali ya  Forum CC imeandaa kongamano la siku moja kwa vijana kutoka  Asasi za kiraia lililojadili msimamo wa Tanzania juu ya masuala ya Mazingira, hususan Mabadiliko ya Tabianchi  kuelekea Mkutano Mkubwa wa Mazingira Duniani utakaofanyika katika jiji la Lima nchini Peru, Desemba 2014. 
 Sehemu ya Washiriki walioshiriki katika kongamono hilo la siku moja lililoandaliwa na Taasisi isiyo ya kiserikali ya Forum CC wakifuatilia mjadala kwa makini.
 Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh. Ummy Mwalimu (wa pili kulia) akijibu maswali ya washiriki katika kongamano la vijana jijini Dar es Salaam katika Hotel ya JB Belmont. Kongamano hilo la siku moja lililenga kukusanya maoni ya vijana na kuainisha changamoto katika suala zima la Hifadhi ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi.
 Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh. Ummy Mwalimu (wa kwanza kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa kongamano hilo. Wengine katika picha, (waliokaa) ni Bi. Grace Munna, Mkurugenzi wa Program kutoka Forum CC.
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh. Ummy Mwalimu akiongea na waandishi wa habari  (hawapo pichani) mara baada ya kufungua kongamano hilo.

No comments: