Advertisements

Wednesday, November 19, 2014

LA VEDA ATINGA GLOBAL, APANGUA SKENDO YA KUJICHUA






La Veda akiwa na Saxaphone yake wakati akifanyiwa Exclusive Interview kwenye studio za Global TV Online jana.
La Veda akipozi na mama yake mzazi, Mecky Vedastous ndani ya studio za Global TV Online zilizopo ndani ya Global Publishers.

La Veda wakati wa Exclusive Interview na Global TV Online.
La Veda akipozi na Mhariri wa Gazeti la Ijumaa Wikienda, Sifael Paul.
...Akipozi na Mhariri wa Gazeti la Championi Ijumaa, John Joseph.
...La Veda akiwa na Mhariri wa Gazeti la Risasi Jumamosi, Erick Evarist.
La Veda akiwa na Shafii Mohammed wa Kitengo cha IT.

La Veda akiwa na Clarence Mulisa ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari (IT) wa Global Publishers.

La Veda akiwa na Mcharaji Katuni wa Global, Aloys Jacob.

...Akiwa na Mwandishi wa Championi, Martha Mboma.



La Veda akionyesha umahiri wake wa kupiga Saxaphone.
La Veda (wa pili kulia) akipozi na Mama yake Mecky (wa pili kushoto), Sifael Paul (wa kwanza kushoto) na Mdau Ayoub (wa kwanza kulia).

KWA mara ya kwanza baada ya kukaa kimya kwa muda tangu atoke katika shindano la Big Brother Africa 'BBA', mshiriki aliyekuwa akiiwakilisha Tanzania katika Jumba la Big Brother Africa 2014, Irene Neema Vedastous 'La Veda' jana amefanya Exclusive Interview na Global TV Online ambapo amefunguka mambo kibao ikiwemo kukanusha skendo iliyozagaa ya kujichua akiwa mjengoni.

La Veda amesema hakufanya kitendo hicho na kufafanua kuwa ilikuwa uzushi ndani ya jumba hilo kutoka kwa baadhi ya washiriki ili waweze kumtoa katika mashindano hayo.

Mrembo huyo ameelezea pia malengo yake ya baadaye na jinsi alivyojipanga kutimiza mipango yake ya muziki, mitindo na filamu.

Mbali na hayo, La Veda aliachia singo yake mpya ya wimbo uitwao Let It Go ambayo imeingia mtaani jana.Credit:GPL

No comments: