ANGALIA LIVE NEWS

Wednesday, December 10, 2014

Jaji akubali rufaa dhidi ya Pistorius

Kiongozi wa mashitaka aliyewasilisha kesi ya rufaa dhidi ya Pistorius

Mahakama nchini Afrika Kusini imemruhusu kiongozi wa mashitaka kukata rufaa dhidi ya kosa alilopatikana nalo hatia Oscar Pistorius la kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.

Kesi hio, sasa itaanza kusikiliza katika mahakama ya juu zaidi upande wa mashitaka ukitaka Pistorius ahukumiwe kwa kumuua mpenzi wake kwa kusudi.Oscar Pistorius

Jaji Thokozile Masipa, alisema hataruhusu rufaa dhidi ya hukumu iliyotolewa ya miaka mitano dhidi ya Oscar mwezi Oktoba.

Kiongozi wa mashitaka Gerrie Nel aliambia mahakama kuwa hukumu hio ni ndogo sana ikilinganishwa na kosa la OscarBBC

No comments: