Advertisements

Sunday, December 21, 2014

RAIS OBAMA ASIFU UVAAJI WA FULANA YA I CAN'T BREATHE ALIYOVAA MCHEZAJI WA KIKAKPU LEBRON JAMES

LeBron Obama
Rais wa Marekani Mhe. Barack Obama amesifia uvaaji wa fulana wa mchezaji wa mpira wa kikapu Lebron James wakati alipokua akifanyiwa mahojiano na gazeti la the people magazine. Rais Barack Obama alipouliwa swali hilo nini mtizamo wake alisema nadhani ni jambo zuri kwa mchezaji huyo na wengine waliopaza sauti zao kuwakilisha mawazo yao kwa mambo yaliyotokea ya kuuwawa kwa Wamarekani weusi na polisi huko Ferguson jimbo la Missouri na Brooklyn New York na baadae mahakama kuwaachia huru polisi hao waliofanya mauaji hayo kwamba walikua wakitekeleza wajibu wao wa kazi.

I can;t Breathe ni maneno ya mwisho aliyeongea Eric Garner kabla ya kukata roho baada ya kukabwa koo na polisi wakati walipokua wamekwenda kumtia mbaroni.

No comments: