ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, February 12, 2015

SHANGAZI WA BOBBI KRISTINA ASEMA HABARI ZA KUONDOLEWA MASHINE NI ZA UWONGO

Habari za kuondolewa mashine anayotumia Bobbi Kristina ili aendelee kuishi si za kweli habari hizo zilizokuwa zimezagaa kwenye mitandao ya kijamii ndani na nje ya Marekani zilisema familia ya Bobbi Kristina ilikubaliana iondoe mashine ili mtoto huyo wa afe siku moja na ile aliyokufa mama yake Whitney Houston Februari 11 kitu ambacho shangazi huyo wa Bobbi Kristina amekataa na kusema si cha kweli.

Bobbi Kristina alikutwa ameanguka bafuni huku kichwa kikiwa kikiwa ikimeinamia chini na kuonekana na michubuko kitu ambacho kimepelekea polisi kufanya uchunguzi wao kwa kumhoji mchumba wake Nick Gordon na rafiki yao aliyekuwepo siku ya tukio. Nick Gordon ni mtoto aliyelelewa na Whitney Houston tangia alipokua na miaka 9 na kuingia na mahusiano ya mapenzi na Bobbi Kristina ambaye ni mtotoi wa Whitney Hoston aliyezaa na Bobby Brown. Marafiki wa wawili hao wamedai wapenzi hawa wameishakua na maugomvi huko nyuma kitu wanachodai ni kutokana na wivu alionao Nick Gordon kwa Bobbi Kristina.

Shangazi wa Bobbi Kristina aliomba Dunia waendelee kumwombea Bobbi Kristina aendelee kupata nafuu na kupona kabisa kwani imekuwa ni wakati mgumu kwa familia na maumivu hasa kwa baba yake Bobby Brown. Bobbi Kristina bado yupo kwenye mashine katika hospitali ya chuo kikuu cha Emory jimbo la Georgia.

No comments: