Advertisements

Saturday, March 21, 2015

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA AVISHA YEO MAAFISA WA JESHI LA MAGEREZA, JIJINI DAR ES SALAA

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja akikagua Gadi Maalum ya Heshima iliyoandaliwa na Maafisa wa Jeshi la Magereza katika hafla ya uvishaji vyeo kwa Maafisa waliopandishwa vyeo ngazi mbalimbali(jana) Machi 20, 2015 katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Dar es Salaam.
Bendi ya Jeshi la Magereza ikipita mbele ya Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) kutoa heshima baada ya zoezi la uvishaji vyeo Maafisa 77 wa vyeo mbalimbali kukamilika.
Maafisa wa Jeshi la Magereza Nchini pamoja na Wageni Waalikwa wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mgeni rasmi, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) katika hafla ya zoezi la uvishaji vyeo kwa Maafisa 77 wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza(CGP), John Casmir Minja akimvisha cheo cha Kamishna Msaidizi wa Magereza, Afisa Mwandamizi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
Jeremiah Katungu katika hafla ya uvishaji vyeo kwa Maafisa waliopandishwa vyeo ngazi mbalimbali(jana) Machi 20, 2015 katika Viwanja ya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Wanawake vyeo mbalimbali(waliosimama nyuma) baada ya zoezi la uvishaji vyeo hivyo Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam(wa pili kushoto) ni Kamishna Huduma za Urekebishaji, Injinia Dionice Chamulesile(wa pili kulia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga(wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Erasmus Kundy. Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza.

Na Lucas Mboje, Dar es Salaam;
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini(CGP), John Casmir Minja amewavisha yeo Maafisa wa Jeshi la Magereza 77 wa Mkoa wa Dar es Salaam kati ya 292 waliopandishwa yeo mbalimbali nchi nzima.

Hafla ya uvishaji yeo hivyo imefanyika(jana) Machi 20, 2015 katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya zoezi la uvishaji yeo kwa Maafisa hao Jenerali Minja alisema "kutunukiwa vyeo hivyo kulizingatia uzoefu kazini na utendaji kazi mzuri".

Vigezo vingine ni elimu, ujuzi na jinsia ambapo kati ya Maafisa 292 waliopandishwa vyeo nchi nzima Maafisa Wanawake ni 37 sawa na asilimia 13.

"Idadi ya Maafisa Wanawake Jeshini ni ndogo lakini tumeanza kuwapandisha Maafisa Wanawake kuanzia vyeo vya chini ili kuleta uwiano unaotakiwa" alisema Jenerali Minja.

Aidha, Jenerali Minja aliongeza kuwa vigezo vingine vilivyotumika kuwapandisha vyeo hivyo ni uwezo wa kumudu Madaraka zaidi pamoja na kuwepo kwa nafasi kwa cheo husika

Tume ya Polisi na Magereza katika kikao chake Namba 2/2014/2015 kilichofanyika Machi 16, 2015 chini ya Mwenyekiti, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Pereira Ame Silima kimewapandisha vyeo jumla ya Maafisa 292 wa Jeshi la Magereza kuanzia Machi 16, 2015.

No comments: