Thursday, March 12, 2015

PITA PITA YA VIJIMAMBO UDC

T.E.S ndani ya University of the District of Columbia kufunga machine ya kukaushia matunda, na pia machine hiyo ina uwezo wa kukausha samaki. Mradi huu unasimamiwa na World Bank kwa ajili ya chuo hicho na maalum kwa wanafunzi kutoka West Africa watakao kuja chuoni hapo na kujifunza jinsi ya ukaushwaji wa matunda na samaki kwa njia ya moshi.
Dr Temba wa Brooklyn New York ni Engineer na kampuni yake ya Temba Engineering Service ni Mtanzania anaeunda machine hizo, na Chuo cha (UDC) kimempa tenda ya kufunga machine hii kwa ajili ya wanafunzi. Tanzania pia inaitaji kutambua na kuheshima wataalam wasomi walio ughaibuni na kuwapa nafasi ya kutumia taaluma yao kwa manufaa ya nchi. Hii ni sehem # 3 sehem #4 na ya #5 tutawajuza hapa hapa Vijimambo.

No comments: