Advertisements

Sunday, April 19, 2015

KIWANDA CHA TUMBAKU MOROGORO CHAFANYA SHERERE KUFUNGA NA KUFUNGUA MSIMU MPYA‏

Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC), David Crowhorst akikabidhi zawadi kwa wafanyakazi waliofanya kazi kwa muda mrefu ambao wamefanya kazi kwa zaidi ya miaka 15 mfululizo.
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC), David Crowhorst akitoa hotuba yake wakati wa sherehe za kumaliza msimu uliopita na kukaribisha msimu mwingine pamoja na kutoa zawadi kwa wafanyakazi waliotumikia kampuni hizo kwa muda mrefu pamoja na wafanyakazi bora zilizofanyika kiwandani hapo. Katika hotuba yake mkurugenzi huyo alisema makampuni hayo yamesaidia Mkoa wa Morogoro kuanza kuinuka kiuchumi kutokana na kutoa ajira za msimu takribani 3000 kila mwaka na kusaidia kupunguza matatizo ya uhalifu yaliyokuwa yakifanywa na vijana wasio kuwa na shughuli za kujiingizia kipato. 

David Crowhorst akiwapakulia chakula waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa tafrija hiyo.
Mkurugenzi wa Ufundi wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC), Henry Lembert akiwahudumia wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa sherehe ya kufunga msimu.
David Crowhorst akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho.
Picha ya pamoja ya waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda cha tumbaku mkoani Morogoro

No comments: