ANGALIA LIVE NEWS

Monday, June 22, 2015

MWANA DIASPORA KUTOKA MAREKANI, JOHN MASHAKA NI MFANO WA KUIGWA

Taasisi ya John Mashaka Foundation pamoja na American Engineering Group (AEG) hatimaye imeweza kuwasaidia wanakijiji 3,500 katika kijiji cha Manila wilayani Rorya kupata maji safi na salama.  Mradi huu umegharamu kiasi cha Shilling Billion moja. Kabla ya huu mradi wananchi wa hiki kijiji walikuwa wakitembea kilometa 24 kwenda ziwani na kurudi. Kazi ambayo ilikuwa ikifanywa na watoto pamoja ba wanawake.

Huu  ni mradi wa aina yake, kwani unatoa maji safi na salama. Na ina uwezo wa kusafisha kiasi cha lita 100,000 kwa siku ambayo inakuwa safi na salama. Kwa kiwango cha 99.9%. Mitambo hii imeagizwa moja kwa moja kutoka Marekani, ambaki ilibuniwa kwa namna yoyte ile ile. Inajitegemea na kujiendesha kwa kutumia nishati ya jua. Pampu ya maji ina uwezo wa kufanya kazi kwa miaka 20.
Wakina mama watakao simamia mradi wa maji wakipiga picha pamoja mbele ya matenki ya maji

Mafundi wakishauriana jamba. Huu mtambo unaweza kupandisha maji lita 20,000 kwa saa. Hufanya kazi kwa kutumia solar. Na unachuja maji kwa 99.99% kuwa safi na salama

 Mkuu wa mkoa wa Mara, Col. (Rtd) Aseri Msangi akiongea na wanakijiji kuhusu manufaa ya huu mradi wa maji kwenye maisha yao



 Mafundi wakichota maji kwenye kisima cha zamani, ambayo yalikua ya msimu
Mafundi wakishauriana jamba. Huu mtambo unaweza kupandisha maji lita 20,000 kwa saa. Hufanya kazi kwa kutumia solar. Na unachuja maji kwa 99.99% kuwa safi na salama


2 comments:

Anonymous said...

Safi sana Mungu ambariki

Anonymous said...

Kitu simple kama kuvuta maji na pump hadi msaada wa Wazungu? Mxxhhh!