ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, June 21, 2015

WAZIRI WA ARDHI WILLIAM LUKUVI AZINDUA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU ZINAZOJENGWA NA NHC WILAYANI MASASI

New Picture (5)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi akipewa maelezo ya mradi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Masasi na Kaimu Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki wa NHC Bw. Haikamen Mlekio.
New Picture (4)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi akiweka jiwe la msingi katika nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Masasi ambazo ujenzi wake utakamilika mwezi Oktoba mwaka huu.
New Picture (3)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi akisalimia viongozi wa NHC mara baada ya kuwasili eneo la Napupa Masasi kuzindua nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC. Anayemuongoza Mh. Waziri ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Felix Maagi.
New Picture (7)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mh. William Vangimembe Lukuvi akiongea na hadhira iliyofurika katika sherehe za uzinduzi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Masasi.Alizitaka taasisi zinazotoa huduma ya umeme na maji kutekeleza majukumu yao ili kupunguza gharama za uuzaji wa nyumba zinazojengwa na waendelezaji wote wa makazi.
New Picture (8)
Sehemu ya umati wa wananchi waliohudhuria sherehe za uzinduzi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Masasi.

No comments: