Advertisements

Monday, August 31, 2015

PSPF WATOA ZAWADI KWA WASHINDI WA LIGI YA MADEREVA WA BODABODA WA KIPUNGUNI JIJINI DAR

 Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma(kushoto) akikabidhi jezi kwa kapteni wa timu ya G Unity Fc kwa ajili ya mchezo wa fainali uliofanyika katika kiwanja cha Kipunguni B katika kata ya Kipunguni manispaa ya Ilala jijini Dar. Ambapo timu ya G Unity FC waliibuka washindi baada ya kuichapa timu ya Sukuma Land Fc bao 5 kwa 2.
  Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma(kushoto) akikabidhi jezi kwa kapteni wa timu ya Sukuma Land FC wakati wa mchezo wa fainali wa kombe la Madereva bodaboda wa kata ya Kipunguni.Wa pili kushoto ni ASP Mbunja Matibu kutoka Traffic Makao Makuu.
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Eliaichi Remmy(kushoto) akitoa somo kwa madereva bodaboda kuhusu Mfuko wa Pensheni wa PSPF hasa katika uchangiaji wa Hiari(PSS) waliofika katika mchezo wa fainali katika uwanja wa Kipunguni B
Mmoja wa Madereva Bodaboda akiendelea kupewa faida za mfuko wa Uchangiaji wa Hiari(PSS) kutoka kwa Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma(kushoto)
Mmoja wa madereva wa Bodaboda akijisajili kwenye mfuko wa (PSPF) kupitia (PSS) kwa ajili ya kuendelea kupata huduma zilizobora na  zenye uhakika kulia ni Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Eliaichi Remmy 
Mmoja wa madereva wa Bodaboda akijiunga kwenye mfuko wa (PSPF) kupitia (PSS) ambapo kila mtu anaweza kujiwekea akiba kupitia kwenye mfuko huo wa hiari wakati wa mchezo wa fainali.
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Eliaichi Remmy(kushoto) akiwasajili madereva wa Bodaboda kwenye mfiko wa Uchangiaji wa Hiari(PSS)  wakati wa mchezo wa fainali wa Madereva bodaboda ambapo G Unity aliibuka mshindi kwa kumchapa Sukuma Land bao 5-2

Vijana waliofika katika mchezo wa fainali wakisoma vipeperushi vya mfuko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ambapo mfuko huo ulidhamini ligi hiyo iliyoendeshwa kwa wiki nzima
Mmoja wa Madereva Bodaboda akisoma maelekezo ya jinsi ya kutuma pesa kwenye akaunti kwenye mfuko wa Uchangiaji wa Hiari(PSS) mara baada ya kupatiwa kitambulisho cha uanachama wa mfuko wa PSPF.
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Eliaichi Remmy(kushoto) akimjazia fomu ya mfuko wa Uchangiaji wa Hiari(PSS) mama aliyekuja kushabikia timu yake wakati wa fainali ya Kombe la Madereva bodaboda
Maafisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF,waratibu wa michezo hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Timu ya Sukuma Land ambapo katika mchezo huo timu hiyo iliibuka mshindi wa pili baada ya kufungwa na timu ya G Unity Fc kwa mambao 5-2.
 
Maafisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF wakiwa kwenye picha ya pamoja na waratibu wa michezo hiyo pamoja na Timu ya G Unity Fc walioibuka washindi wa wa kwanza baada ya kufunga timu ya Sukuma Land Fc mabao 5 -2, mchezo huo uliofanyika katika kiwanja cha Kipunguni B
Mchezaji wa Timu ya Sukuma Land Fc akiwatoka mabeki wa G Unity Fc ambapo katika mchezo huo timu ya G Unity Fc iliibuka mchindi wa mashindano hayo
Ilikuwa ni burudani katika mchezo wa fainali kati ya Timu ya G Unity Fc na Sukuma Land Fc
Gori kipa wa timu ya G Unity FC akijifunga gori wakati wa mchezo wa fainali uliopigwa kwenye uwanhja wa Kipunguni B
Wachezaji wa Timu ya G Unity Fc wakishangilia baada ya kupata bao wakati wa mchezo wa fainali

Mbwembwe za mashabiki katika fainali hizo
Hizi ndizo zawadi zilizotolewa na Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwa mshindi wa kwanza mpaka wa nne katika mashindano ya mpira wa miguu kwa madereva bodaboda wa kata ya Kipunguni amabapo mshindiwa kwanza aliondoka na Mbuzi wawili na seti moja ya jezi, mshindi wa pili aliondoka na mbuzi mmoja na seti moja ya jezi, mshindi wa tatu aliondoka na seti moja ya jezi na mshindi wa nne aliodoka na mpira mmoja.
Mkurugenzi mtendaji wa kata ya Kipunguni na Kivule Dr. Kadry Pinde ambaye alikuwa ni Mgeni rasmi katika mchezo wa fainali akikabidhi mpira kwa kapteni wa timu ya Kilimani Fc walioibuka washindi wa wa nne katika mashindano ya mpira wa miguu kwa madereva Bodaboda wa kata ya Kipunguni. Wa kwanza kushoto ni Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma.
Mkurugenzi mtendaji wa kata ya Kipunguni na Kivule Dr. Kadry Pinde akiwakabidhi zawadi ya seti ya jezi timu ya Loliondo Fc baada ya kuibuka mshindi wa Tatu katika mashindano hayo.
Kapteni wa timu ya Sikuma Land Fc akipokea seti ya jezi mmoja na Mbuzi mmoja baada ya kuibuka washindi wa pili katika mashindano ya mpira wa miguu kwa madereva bodaboda kutoka kwa Mkurugenzi mtendaji wa kata ya Kipunguni na Kivule Dr. Kadry Pinde ambaye alikuwa mgeni rasmi katika fainali hiyo. Wa kwanza kushoto ni ASP Mbunja Matibu kutoka Traffic Makao Makuu, wa pili kushoto ni Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Eliaichi Remmy
Washindi wa mashindano ya mashindano ya mpira wa miguu kwa madereva Bodaboda wa kata ya Kipunguni wakisalimiana mgeni rasimi wakati wa kukabidhiwa zawadi zao
Mkurugenzi mtendaji wa kata ya Kipunguni na Kivule Dr. Kadry Pinde akikabidhi seti ya jezi na mbuzi wawili wa kapteni wa timu ya G Unity Fc ambao waliibuka washindi wa mashindano ya mpira wa miguu kwa madereva Bodaboda wa kata ya Kipunguni baada ya kuichakaza timu ya Sukuma Land Fc bao 5-2




MAshabiki wakiendelea kufuatia kinachijiri uwanjani

Mashindano ya ligi wa mpira wa miguu kwa madereva bodaboda yahitimishwa na wadhamini wa mashindano hayo ambao ni mfuko wa Pensheni wa PSPF kwa kuweza kuwasajiri wachezaji katoka mfuko wa hiari wa PSS. Ligi hiyo iliyodumu ndani ya siku saba (7) ambapo alikuwa akitafutwa mshindi atakayeweza kuwa balozi mzuri wa mfuko wa penshenI wa PSPF yamemalizika kwa timu 32 kumenyana vikali na timu  ya G Unity kuibuka kinara ambapo timu hiyo ndiyo iliyotawazwa na kuwa balozi wa PSPF katika kata ya Kipunguni  mara baada ya fainali iliyohusisha timu ya Sukuma Land FC na G Unity Fc na hatimaye timu yaG Unity kuibuka kinara kwa bao 5 kwa2 katika fainali iliyopigwa katika kiwanja cha Kipunguni B.

Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma alikabidhi jezi za kuchezea fainali kwa timu mbili zilizo fuzu kuingia katika fainali hizo ambazo ni G Unity Fc na Sukuma Land FC alisisitiza wachezaji wote kuweza kijiunga na mfuko wa pensheni wa PSPF fainali hizo za mashindano hayo ya ligi ya madereva bodaboda wa Kipunguni ambayo yaliweza kuhitimishwa na Mkurugenzi mtendaji wa kata ya Kipunguni na Kivule Dr. Kadry Pinde ambapo aliweza kuwaasa vijana waweze kujihusisha na kufanya kazi kwa bidii na kuweza kuhifadhi mafao yao katika mfuko wa pensheni wa PSPF.

Msaidizi wa Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Josephat Sylvery Tirumanywa naye alitoa neno kuhusu usalama barabarani na kuwashukuru wachezaji kwa kucheza ligi hiyo kwa usalama na kumalizika kwa amani na hata hivyo aliwasisitizakuwa watu wote wanaotumia vyombo vya moto kuwa makini pindi wawapo barabarani.

No comments: