
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Luteni mstaafu Chiku Gallawa akisalimiana na viongozi wa Chama cha Wasambazaji maji(AWAC) pamoja na wadau mbalimbli wa maji mara baada ya kuwasili hotelini hapo kwa ajili ya ufunguzi wa kongamano.(Picha na John Banda wa Pamoja Blog)

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Luteni mstaafu Chiku Gallawa akizungumza jambo kwenye ufunguzi wakongamano la wadau wa maji lililoandaliwa na Chama cha wasambazaji wa maji (AWAC) na linalofanyika kwa siku tatu ili kujadili namna ya kupunguza uharibifu wa vyanzo vya maji.




Wadau mbalimbali wakijadili namna ya kupunguza uharibifu wa vyanzo vya maji katika kongamano la wasambazaji wa maji lililofanyika katika ukumbi wa St. Gaspar mkoani Dodoma.

Wadau mbalimbali wa maji wakifatilia kwa makini kongamano lililoandaliwa na hama cha wasambazaji wa maji (AWAC) na kufanyika katika hotel ya St. Gasper mkoani Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Luteni mstaafu Chiku Gallawa(kulia) akibadilishana mawazo na wadau wa maji mara baada ya kumaliza kufungua kongamano la kujadili namna ya kulinda na kuvitunza vyanzo vya maji linalofanyika kwa siku tatu mjini humo.

Wafanyakazi wa Chama cha wasambazaji wa maji (AWAC) wakiwa kwenye picha ya pamoja katika viwanja vya St. Gaspar mjini Dodoma kwa ajili ya kongamano la Maji

Afisa habari wa shirika la viwango Tanzania, Neema Mtemvu(kulia) pamoja na afisa mwenzake wa shirika la Viwango Tanzania wakiendelea kutoa elimu kwa wadau hao wa maji nchini waliofika kwenye kongamano la kujadili namna ya kulinda na kuvitunza vyanzo vya maji lililofanyika katika Hotel ya St. Gasper mkoani Dodoma.


Picha ya Pamoja
No comments:
Post a Comment