Advertisements

Thursday, November 26, 2015

KAMPUNI YA MEGATRADE INVESTMENT LTD YAKIPIGA JEKI CHUO KIKUU CHA USHIRIKA NA BIASHARA MOSHI PAMOJA NA CHAMA CHA SOKA CHA MKOA WA KILIMANJARO

Meneja masoko wa Kampuni ya Megatrade Investment ya jijini Arusha,Edmund Rutaraka akimkabidhi hundi ya kiasi cha shilingi Milioni 1.5 ,katibu wa Chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro ,KRFA,Mohamed Musa kwa ajili ya kusadia ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa iliyoanza hivi karibuni.
Mweka hazina wa Chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro,Kusianga Kiata,akitizama hundi iliyotolewa na kampuni ya Megatrade Investment ya jijini Arusha.a

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
Baadhi ya wadau wa soka waliofika kushuhudia makabidhiano hayo yaliyofanyika katika ofisi za chama hicho zilizopo jengo la Voda House.
Meneja Masoko kanda ya Kaskazini ,Edmund Rutaraka akimkabidhi Makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Ushirika na Biashara ,Moshi,( MOCU),Profesa Faustine Bee hundi ya kiasi cha shilingi Mil 2 kusaidia maeneo mbalimbali yenye changamoto chuoni hapo.
Meneja Masoko wa kampuni ya Megatrade Investment ya jijini Arusha,Edmund Rutaraka akizungumza jambo mara baada ya kukabidhi hundi kwa mkuu huyo wa chuo.
Makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Ushirika na Bashara (MOCU) Profesa Faustine Bee akizungumza mara naada ya kukabidhiwa hundi hiyo.

No comments: