Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi jijini Mbeya, mapema mchana wa leo wamekamata bidhaa zilizoingizwa nchini kimagendo kupitia mpaka wa Tunduma. Bidhaa hizo ni vinywaji aina ya Dragon vilivyokuwa vikisafirishwa na gari aina ya Toyota Hiace. Pichani ni Kamanda wa Polisi Mkoani wa Mbeya, SACP Ahmed Msangi (akiwasiliana kwa njia ya simu) akiwa pamoja na Afisa wa TFDA Kanda ya Nyanda za juu kusini, Peter Namaumbo.



No comments:
Post a Comment