Advertisements

Thursday, May 26, 2016

MAMBO 10 UNAYOTAKIWA KUYAJUA KUHUSU MCHUMBA WAKO KABLA HAMJAOANA

Unadhani kuwa unajua kila kitu kuhusu mume wa maisha yako? Mahusiano mengi hukoma kwa sababu ya masuala ya mawasiliano, uongo au shakhsia zisizoendana. Mengine hufikia kikomo kwa sababu wanandoa hawakuchukua muda kujuana.
Famasia yako ya Ndoa Maridhawa imekuletea mambo 10 ambayo unatakiwa kuyajua kuhusu mwanaume wa maisha yako kabla hujachukua hatua zaidi. Iwapo unayajua baadhi, basi endelea kufuatilia zaidi na zaidi:
1. MALENGO YA KWELI YA KAZI YAKE
Huwenda unaijua kazi yake… lakini unajua kuhusu kazi ya ndoto yake? Unajuaje iwapo atabadili kazi yake baada ya miaka 5? Tambua mapema iwapo mumeo anataka kuwa meneja, kibarua au mkurugenzi wa kampuni au shirika. Anaweza akawa na wazo la kumiliki biashara zake mwenyewe.

2. RADIAMALI YAKE (reaction):
Mzee wangu mmoja aliwahi kuniambia: “Unaweza kujua kuhusu mtu fulani kwa kutazama namna anavyoshughulikia mambo”. Kauli hii inatufundisha kujua kuhusu ghadhabu, hasira na subira ya mtu husika. Hili linaweza kukuonesha namna mtu huyo alivyo. Kupitia radiamali ya mtu ndipo unapoweza kujua silka yake. Lizingatie hilo.

3.   ENEO ANALOPENDA ZAIDI DUNIANI
Tambua eneo analolipenda zaidi katika maisha yake, na ambalo humpatia furaha zaidi. Wakati fulani utaweza kutumia fursa hiyo kumfanya kuwa mwenye furaha.
Kwa mfano, mimi ninapenda sana mkoa wa Kigoma… Sio tu kwa sababu ni kwetu, lakini kwa sababu kuna mambo mengi yenye kuijaza kumbukumbu ya maisha yangu kiasi kwamba huhisi ombwe nisipoyaona mambo hayo.

4.   VIWANGO VYA MAISHA YAKE
Jitahidi sana kujua “living standard” yake kabla ya kuingia katika ndoa. Hilo litakusaidia kujua aina ya mtu unayeingia naye kwenye ndoa na jinsi ya kuamiliana na hali zenu za kiuchumi.


No comments: