Advertisements

Friday, May 20, 2016

SAGCOT IHEMI CLUSTER YAFANYA MKUTANO NJOMBE

Mkuu wa mkoa wa Iringa akichangia mada
Mkuu wa Wilaya Iringa Mhe. Kasesela akichangia mada
Mkuu wa wilaya Iringa, Mkuu wa mkoa Iringa, Spika mstaafu bi Ana Makinda na Mkuu wawilaya ya Mfundi wakisikiliza mada
Mkuregenzi Mtendaji wa SAGCOT akitoa mada

Wadau wakisikiliza
Mkuu wa wilaya Ludewa Anatory Choya




Picha ya pamoja.

SAGCOT Kongai ya ihemi imefanya Mkutano wake wa tathmini wa yale walio kubaliana katika kukuza uhusiano kati ya sekta binafsi na seriakali katika kuendelaza uwekezaji. Mkutano huo wa siku 2 uliomalizika Njombe leo tarehe 20/05.16. Uliudhuriwa na Mkuu wa mkoa wa Iringa na wakuu wa wilaya za Ludewa, Wanging'ombe, Mufindi, Kilolo na Iringa Mjini uliandaliwa na kituo cha SAGCOT chini ya Mkurugenzi Mtedaji Geofrey Kilenga. Kongai (CLUSTER) ya Ihemi walijadili masuala ya uzalishaji, usafirishaji, Usindikaji pamoja na utafiti katika kukuza uwekezaji na kipato cha wananchi. Sekta binafsi ilihudhuriwa na makampuni makubwa yanayo jihudisha na kilimo pamoja na ufugaji kama ASAS, Darsh INDUSTRIES (RED GOLD), muungano wa wafugaji Ngombe Njombe. 

Pia Bi Neema Mwingu kutoka World Bank alitoa mada yenye kuonyesha kuwa Benki ya Dunia imetenga kiasi cha dola za kimarekani Milion 70 kukuza sekta binafsi inayokua (SME) ili waweze kushirikiana na wewekezaji wakubwa katika mnyororo wa thamani. 

Mapema Mkuu wa Mkoa wa Njombe akiwakilishwa na Mkuu wa wilaya ya Ludewa Bwana Anatoly Chonya alisema Mikoa ya Njombe na Iringa ndio mikoa ambayo ikifanya vizuri katika kilimo na ufugaji basi tanzania itakuwa imeongeza pato la taifa maradufu, aliwaomba SAGCOT kuhakikisha wanazidisha juhudi za kukuza kilimo katika mikoa hiyo. Naye Mkuu wa Mkoa wa Iringa bi Amina Masenza alisistiza suala la sekta binafsi kuhemshimu makubaliano ya awali hasa ya kunufaisha wanannchi walio wakuta, pia alichukizwa na mtindo wa makampuni hayo kuhamisha ulipaji wa kodi ya mapato kwenda Dar es salaam jambo ambalo linapunguza pato la mkoa kwa kiwango kikubwa. Naye Mkuu wa wilaya ya Mufindi Bwana Jolwika Kasunga akichangia alisema " wawekezaji wana kuwa karibu sana na serikali mwanzoni wakati wa kuhangaikia vibali wanapo fanikiwa wanapotea mpaka wapate shida ingine" . 

Naye Mkuu wawilaya ya Iringa Richard Kasesela alisistiza suala la masoko na wawekezaji kupata social licence kutoka katika jamii kabla ya kuanza uwekezaji hili litapunguza sana migogoro isiyo kuwa ya lazima. Katika mkutano huo pia Mkurugenzi wa Sagcot Catalyst Fund alisema lazima sasa wakulima wadogo wawe matajiri la msingi ni kuhakikisha fedha zote hizi zinawanyanyua na kuwafanya matajiri.

No comments: