Wednesday, June 8, 2016

Ninavyoishi na Aunt Ezekiel ni ndoa tosha – Mose Iyobo

Dancer maarufu wa Diamond, Mose Iyobo amesema jinsi anavyoishi na Aunt Ezekiel ni ndoa tosha lakini atafunga ndoa ili watu wa verify kama instagram.
Mose Iyobo na Aunt Ezekiel wamefanikiwa kupata mtoto mmoja [Cookie] mwenye umri wa mwaka mmoja.
Akiongea kwenye kipindi cha E News, kinachoruka kupitia EATV, Iyobo alisema, “Lakini ninavyoishinae ni ndoa tosha kwa sababu tunaishi kama baba na mama hivyo nataka kujithibitisha inabidi nifunge ndoa ili watu wani-verify kama instagram.”

Aidha Iyobo ameongeza kuwa hapendi watu wanavyomzungumzia vibaya mzazi mwenzie huyo wakidai kuwa eti ni mzee kwani angelikuwa hivyo yeye asingelisogea kwa kuwa angelikuwa kama anatembea na mama yake.

No comments: