Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda
cha Goodwill Ceramic, Frank Yang (aliyeshika kipaza sauti) wakati
akiangalia ramani ya kiwanda hicho katika
kijiji cha Mkiu Mkuranga Pwani juzi.kulia ni Mbunge wa Jimbo la Mkuranga
Abdalah Ulega
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea mfano wa hundi ya Sh 20 milioni
kutoka kwa Balozi wa China Nchini, Dk Lu Youqing (wa pili kulia)
kusaidia ununuzi wa madawati katika Shule zilizopo katika wilaya ya
Mkuranga. Kulia ni Mbunge wa Jimbo hilo, Abdallah Ulega na Kushoto ni
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage.
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa ujenzi wa viwanda unaotekelezwa kwa kasi hapa nchini utakuwa ndio mwarobaini wa kuondoa tatizo la ajira kwa vijana kwa wingi hapa nakudai kuwa atakayekwamisha mkakati huo wa Serikali hatovumiliwa.
Pia amesema kuwa maeneo yote yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Viwanda hivyo na yale ambayo tayari ujenzi wa viwanda umeshaaza lazima miundombinu ya umeme wa uhakika upatikane ili kuwezesha viwanda hivyo kuzalisha kwa wingi.
Majaliwa aliyasema hayo juzi Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani ikiwa sehemu ya mwendelezo wa ziara yake ya kikazi,ambapo alitembelea utekelezaji wa Ujenzi wa Kiwanda cha Vigae cha Googwill,ambacho kinajengwa katika kijiji cha Kiu,kilichopo Kata ya Nyamato tarafa ya Mkamba wilayani humo.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
No comments:
Post a Comment