Advertisements

Wednesday, August 10, 2016

VIJANA WAENDESHA MDAHALO KUJADILI CHANGAMOTO MBALIMBALI ZINAZOWAKABILI KUELEKEA SIKU YA KIJANA DUNIANI, KARIMJEE JIJINI DAR

Mwakilishi Mkazi msaidizi kutoka UNFPA Bi. Christine Mwanukuzi akifungua mdahalo huo, kuwashukuru vijana kwa kujumuika pamoja na kuwapongeza kwa kufanikisha mdahalo huo kuelekea katika siku ya vijana duniani siku ya tarehe 12.08.2016
Bw. Badru Juma Rajabu akielezea historia ya siku ya vijana ilipoanzia na kusisitiza kuwa vijana wanatakiwa kutambulika na wasisahau kuchukua fursa pale wanapowezeshwa

Oscar Kimario muwezeshaji kutoka Restless Development akielezea baadhi ya ripoti juu ya vijana na kuwasihi vijana kuwa ndio watakuwa mstari wa mbele katika maendeleo endelevu hivyo wanapaswa kujituma na kufanya kazi kwa bidii


Vijana wakiendelea kufuatilia mdahalo huo kwa makini
Mwakilishi kutoka Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa ILO Nancy Lazaro akizungumzia ajira zenye staha ,alisema kuwa vijana wengi wameajiriwa lakini katika ajira zisizo na staha na kusisitiza ifike kipindi sasa vijana waajiliwe na kazi zenye Staha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Msichana Initiatives Rebeca Gyumi akijibu maswali mbalimbali ambayo waliuliza vijana waliofika katika kongamano hilo na kusema kwamba sio kweli kwamba wanafunzi waliomaliza elimu ya vyuo ni vilaza
Vijana wakiendelea kufuatilia wajibu maswali wakijibu yale waliyo yauliza

Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya St.Josephs Veronica Shayo kidato cha tano akisisitiza vijana kuwa na tabia za kuweka akiba kwa kile wanachopata ili kije kuwasaidia pindi watakapo kuwa wakubwa.
Muwezeshaji wakati wa kongamano hilo la vijana ambalo kauli mbiu yake inasema Sepesha Umasikini kwa Michongo Endelevu na yenye tija Bw. Lawrence Ambokile akiendelea kutoa mwongozo 
Noreen Toroka akijibu baadhi ya maswali lakini pamoja na hayo amewasisitiza vijana kuto kutumia kipato wanacho kipata bila tija na wawe na utaratibu wa kuhifadhi kwa ajili ya maendeleo baadae, pia aliongeza kuwa vijana wasilazie damu fursa mbalimbali zinazotolewa kwa ajili yao

Baadhi ya vijana kutoka Restless Development na wanafunzi pamoja na wadau wakendelea kufuatilia mdahalo

Mwanzilishi wa Malkia Investment Bi. Jenipher Shigoli akichangia  jambo katika mdahalo huo

Albert Kutoka ILO akichangia na kujibu maswali ya vijana mbalimbali katika mdahalo huo ambapo alisisitiza vijana kujituma
 Mwanzilishi wa Charity Movement Sophia Mbeyela akitoa ushuhuda wake wa jinsi alivyo anza ujasiliamali tangia akiwa mdogo na kusisitiza kwamba vijana haijalishi ni mzima au ana ulemavu wa viungo vya mwili wake wote wanatakiwa kujumuika pamoja na kufanya kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo ya Taifa

Kijana Onesmo akiwaeleza vijana wenzake kuwa kama wao walemavu wavioungo wanaweza kufanya mambo makubwa iwaje vijana wazima wasiweze hii ilikuwa ni changamoto

Picha ya pamoja ya Baadhi ya Washiriki wa Mdahalo huo

Picha na Fredy Njeje wa Blogs za Mikoa



No comments: