Advertisements

Wednesday, September 14, 2016

MUWSA WASAFISHA MIFEREJI YA MAJI TAKA KITUO KIKUU CHA MABASI MJINI MOSHI.

Tope zilizokuwa zimetuama katika mifereji ya kusafirisha maji taka katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi zikiondolewa.
Licha ya kuwepo na kampuni iliyopewa kandarasi ya usafi katika kituo kikuu cha mabasi cha mjini Moshi bado changamoto ya kuziba kwa mifereji ya kusafirisha maji taka imekuwepo .

Wafanyakazi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) walishiriki kuzibua na kuondosha taka zote zilizokuwepo katika mifereji hiyo.
Kitengo cha maji taka cha Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi kilihusika zaidi kuhakikisha hakuna mfereji utakao kuwa umebaki na taka.
Taka ngumu zote ziliondolewa katika mifereji hiyo.
Baadhi ya wafanyabiashara katika kituo hicho kikuu cha mabasi walijitokeza pia katika kusaidia kufanya usafi .
Wafanyakazi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukailisha zoezi la usafi katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: