Advertisements

Monday, September 5, 2016

POLISI KANDA MAALUM DAR WAVUNJA MTANDAO WA MAJAMBAZI.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akizungumza na waandishi habari juu ya operesheni walioifanya na kukamata majambazi watatu katika viwanja vya ofisi ya kanda maalum leo jijini Dar es Salaam.


Na Chalila Kibuda.
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam  limefakiwa kukamata watu watatu wanaodaiwa kuwa ni majambazi hatari  ambao wamekuwa wakishiriki matukio mbalimbali ya uhalifu kwa kutumia silaha.

Watu hao wanaodaiwa kuwa majambazi walipatikana na bunduki 23 za aina tofauti tofauti, Risasi 835, kifaa cha kuzuia risasi kuingia mwilini tatu (Burret Proof), Sare za Polisi, Pingu 48 pamoja na Radio 12 za mawasiliano.

Akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya kanda  maalum, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna, Simon Sirro amesema kuwa majambazi hao walikuwa na mtandao mkubwa ikiwa ni kununua silaha nje ya nchi  kwa ajili ya kufanyia uhalifu katika maeneo mbalimbali.


Kamanda Sirro amesema baada ya tukio hilo timu ya polisi ya upelelezi  iliweka mtego na kufanikiwa kukamata majambazi watatu maeneo ya Mbagala, Keko na Kawe.

Kamanda Sirro amesema katika mahojiano walikiri kufanya tukio katika benki ya Habib African maeneo ya Kariakoo 2014 na Stanbic 2014.

Amesema kuwa majambazi walikiri kuwa na wenzao wako katika msitu wa Vikindu.

CHANZO: MICHUZI BLOG

2 comments:

Anonymous said...

Sahihisho kwa mwandishi: "bullet proof" siyo "burret proof"

Anonymous said...

Mwenzako alikuwa anaandika Kikuryanglish sio English!