Advertisements

Thursday, September 8, 2016

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI CHANIKA WILAYANI HANDENI WAMTUMA MKUU WA WILAYA KUFIKISHA SALAMU ZAO KWA RAIS MAGUFULI

Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe Akifurahia wanafunzi wa darasa la saba mara baada ya kuzungumza nao jambo alikutana nao waliokuwa walipomaliza kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi katika shule ya Chanika wilayani Handeni mkoani Tanga.

Wanafunzi hao wamemwambia Mkuu wa wilaya Mh. Godwin Gondwe kufikisha salamu zao kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli, wakimshukuru kwa kuwezesha elimu ya Msingi mpaka Sekondari kuwa bure , kwani itarahisha wanafunzi wengi ambao wazazi wao hawana uwezo kupata elimu. Wameongeza kuwa "Mtihani ulikuwa mzuri hivyo watafauru kwa kishindo".
Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe Akipiga picha ya pamoja na wanafunzi wa darasa la saba mara baada ya wanafunzi hao kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya Msingi katika shule ya Chanika wilayani Handeni. 
Wanafunzi wa shule ya Msingi Chanika wilayani Handeni wakifurahia jambo mara baada ya kumaliza elimu ya Msingi

No comments: