Advertisements

Thursday, September 15, 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA APOKEA HUNDI YA MILIONI 10 KWA AJILI YA WAATHILIKA WA TETEMEKO

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akipokea mfano wa hundi ya Shilingi milioni 10 kutoka kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (katikati) ikiwa ni mchango wa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera hivi karibuni. Mkutano huo wa kuhamasisha uchangiaji ulifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 13 Septemba, 2016 na kuwashirikisha Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini na Wafanyabiashara. Kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Charles Mwijage na kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Aziz Mlima
Sehemu ya Mabalozi na Wafanyabiashara walioshiriki mkutano huo 
Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa akitoa hotuba wakati wa mkutano wa kuhamasisha uchangiaji kwa maafa yaliyotokea Kagera kufuatia tetemeko la ardhi. 
Sehemu nyingine ya wafanyabiashara akiwemo Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dkt. Reginald Mengi (wa kwanza kushoto) 
Sehemu ya wageni waalikwa walioshiriki mkutano huo wakiwemo Wakurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 
Mhe. Dkt. Kolimba akitoa neno la ukaribisho wakati wa mkutano huo 
Mwenyekiti wa TPSF, Dkt. Mengi akizungumza wakati wa mkutano huo 
Mkutanoo ukiendelea

1 comment:

Anonymous said...

Hili swala la watendaji wa Serikali kuvaa beji za majina yao ingefaa iwe tu wakiwa kazini kwao sio mpaka kwenye hafla za umma.