Advertisements

Thursday, October 20, 2016

TAHADHARI YA UWEPO WA UKAME WA CHAKULA


Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig. Jenerali Mbazi Msuya akifafanua jambo wakati wa Mkutano na waandishi wa habari uliohusu utoaji wa tahadhari ya hali ya Ukame utakaosababisha kukosekana kwa chakula kwa baadhi ya maeneo nchini Oktoba 20, 2016. Mkutano ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano ofisi hiyo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Bw. Paschal Waniha (wa kwanza kushoto) akitoa hoja za masuala ya umuhimu wa taarifa za hali ya hewa katika kujiandaa kukabili maafa wakati wa Mkutano na waandishi wa habari Oktoba 20, 2016. Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Chakula Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Bi. Marystela Mtalo akiwasilisha mada juu ya umuhimu wa kuhifadhi chakula na kulima mazao yenye kustahimili ukame wakati wa mkutano wa waandishi wa habari katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu 20 Oktoba, 2016.  Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: