Advertisements

Friday, November 11, 2016

MKE WA RAIS MAMA JANETH MAGUFULI ARUHUSIWA KUTOKA KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI ALIPOKUWA AMELAZWA

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa anatoka kwenye  Wodi ya Sewahaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kurejea nyumbani  mara baada ya kuruhusiwa baada ya kupata nafuu. Mama Janeth Magufuli alikuwa amelazwa hospitalini hapo tangu tarehe 9 Novemba 2016.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimshukuru Dkt. Raymond Mwenesano, Mkuu wa Idara ya Wagonjwa wa nje na Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili mara baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo na kurejea nyumbani baada ya kupata nafuu.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimshukuru Dkt. Edward Ngwalle, Daktari wa Rais mara baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo na kurejea nyumbani baada ya kupata nafuu.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimshukuru Dkt. Benard Kepha ambaye Daktari Bingwa wa Magonjwa ya dharura na ajali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili mara baada ya kuruhusiwa kutoka na kurejea nyumbani mara baada ya kupata nafuu. Picha na IKULU

3 comments:

Anonymous said...

Hii ajabu kweli kweli. huyu mama kulazwa na kutibiwa nchini kama walalahoi wengine? Kweli nchi inaweza kubadilika. tunamwombea kupona na kuwashukuru madaktari wetu nchini kwa kazi nzuri.

Anonymous said...

Kama mama yetu mke wa RAISI anatibiwa Mhimbili, ni kwanini viongozi wengine wa taifa wanapelekwa nje ya nchi kwa matibabu?????

Anonymous said...

Ina tegemea naugonjwa aliokuwa anaumwa...Ingawaje na mpongeza pia kwa kukubali kutibiwa muhimbili maana wapo wake wa wakubwa hata kichwa kikiuma anaenda Nje