Advertisements

Thursday, November 10, 2016

UMOJA WA MATAIFA WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA

Rais wa IRMCT, Bw. Theodor Meron akiwasilisha mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, hapo siku ya jumatano, Ripoti ya utendaji kazi wa Matawi ya Mahakama za Kimataifa za Kesi za Masalia zinachokua nafasi ya iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ( ICTR) na Mauaji ya halaiki yaliyotokea katika iliyokuwa Yugoslavia ya zamani ( ICTY. Bw. Meron alitumia pia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wa hali na mali katika ujenzi wa majengo yanayochokua nafasi ya ICTR majengo hayo yamejengwa katika eneo la Lakilaki Mkoani Arusha.
Mwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa Ripoti ya utendaji kazi wa IRMCT ambapo alimshukuru kwa namna ya pekee Msajili wa IRMCT Bw. John Hopkins kwa uongozi wake na ushirikiano ambao ameonyesha katika ujenzi wa majengo mapya huko Lakilaki lakini pia katika kusimamia kipindi cha mpito na makabidhiano kutoka ICTR kwenda IRMCT.

No comments: