Advertisements

Wednesday, November 16, 2016

WAZIRI MAHIGA AKUTANA NA WAZIRI WA BISHARA ZA KIMATAUFA NA MAENDELEO WA FINLAND



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Maendeleo wa Finland, Mhe. Kai Mykkanen alipomtembelea kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam. Wawili hao wamezungumzia masuala mbalimbali kuhusu masuala ya biashara, uwekezaji na maendeleo ya huduma za kijamii nchini. Mhe. Kai katika mazungumzo hayo ameahidi kupitia Wizara yake ataendelea kushirikiana na Tanzania katika kuongeza kasi ya ukuaji wa shughuli za maendeleo sambamba na kuendelea kushawishi sekta binafsi za Finland kuja kuwekeza nchini.

Mhe. Waziri, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Maendeleo wa Finland Mhe. Kai Mykkanen 
Mazungumzo yakiendelea 
Mhe. Waziri, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akimsikiliza Waziri wa Biashara za Kimataifa na Maendeleo wa Finland Mhe. Kai Mykkanen walipokutana kwa mazungumzo Wizarani Jijini Dar es Salaam

No comments: