Advertisements

Sunday, May 7, 2017

BW. RAYMOND MUSHUMBUSI NA BI. SUSAN BARNABAS WAFUNGA NDOA KANISA LA MTAKATIFU PETRO OYSTERBAY JIJINI DAR ES SALAAM

Mfanyakazi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Raymond Mushumbusi akiwa pamoja na Mkewe Bi.Susan Barnabas jana wakati walipofunga ndoa takatifu na kuwa mwili mmoja kwenye kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam wakisindikizwa na wasimamizi wao Benedict Mwakasindile na Bi. Leticia Mwakaila , Ndoa hiyo ilifungwa na Padri Padri Haule wa Kanisa hilo Timu nzima ya Fullshangwe inawatakiwa maisha marefu na yenye furaha katika ndoa yenu huku mkijaaliwa kuiongeza dunia.
Bibi harusi Susan Barnabas na msimamizi wake Leticia Mwakaila wakiwa kwenye gari kabla ya kuingia kanisani tayari kwa tukio la kufungwa kwa ndoa hiyo jana.

Mfanyakazi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Raymond Mushumbusi akimvisha pete Mkewe Susan Barnabas wakati walipofunga ndo katika kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jana jijini Dar es salaa.
Mfanyakazi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Raymond Mushumbusi akiwa pamoja na Mkewe Susan Barnabas wakishiriki sala wakati wa ibada ya kufungwa kwa ndoa yao.
Padri Haule wa kanisa la Mtakatifu Petro akiziombe pete za maharusi huku maharusi hao wakiwa wamezishikilia.
Bibi Harusi Susan Barnabas akipozi kwa picha kwenye gari.
Bibi Harusi Susan Barnabas akimvisha pete mumewe Bw. Raymond Mushumbusi wakati walipofunga ndo kwenye kanisa la Mtakatifu Petro Osterbay jijini Dar es salaa huku Padri Haule akishuhudia tukio hilo kulia ni Bw. Benedict Mwakasindile msimamizi wa maharusi hao.
Maharusi wakisaini vyeti vya ndao mara baada ya kufungwa kwa ndoa hiyo.
Maharusi wakiwa kanisani mara baada ya kufungwa kwa ndoa hiyo.
Maharusi wakionyesha vyeti vyao vya ndoa mara baada ya kufungwa kwa ndoa hiyo kwenye kanisa la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam.

No comments: