Advertisements

Sunday, May 14, 2017

TFDA yafungia machinjio 26 Dar

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imeyafungia machinjio 26 kati ya 55 jijini hapa katika Manispaa za Ubungo, Kinondoni, Ilala na Temeke.
Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo amesema hayo leo akizungumza na waandishi wa habari kuwa ukaguzi ulianza Mei 2-12 na kuwahusisha wadau wote muhimu wakiwemo Bodi ya Nyama na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
"Lengo la ukaguzi huo ulikuwa kuangalia utekelezaji wa Sheria ya Chakula, Dawa ya Vipodozi... Ulifanyika usiku kwa machinjio ya ng'ombe na asubuhi na mchana kwa machinjio ya kuku na nguruwe," amesema Sillo.
Amesema katika machinjio 26, moja ni ya ng'ombe, 14 nguruwe na 11 ya kuku.

No comments: