Advertisements

Thursday, June 15, 2017

UNIC Yakutana na Wanafunzi Mbalimbali Kujadili Mkutano wa Baha

Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo akizungumza na baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali na vijana (hawapo pichani) kwenye mkutano kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo akisisitiza jambo kwenye mkutano huo na vijana na wanafunzi kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani.
Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo (mbele) akizungumza na baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali na vijana kwenye mkutano kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Sehemu ya maofisa kutoka Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), wakiwa katika mkutano huo na wanafunzi kutoka shule mbalimbali na pamoja na vijana kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Sehemu ya wanafunzi wakiwa kwenye mkutano huo ulioandaliwa na UNIC, Tanzania kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo (mbele) akizungumza na baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali na vijana kwenye mkutano kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo (mbele) akizungumza na baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali na vijana kwenye mkutano kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo (mbele) akizungumza na baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali na vijana kwenye mkutano kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Baadhi ya wanafunzi wakichangia hoja kwenye mkutano huo ulioandaliwa na UNIC, Tanzania kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Baadhi ya wanafunzi wakichangia hoja kwenye mkutano huo ulioandaliwa na UNIC, Tanzania kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani.

KITUO cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) leo kimekutana na baadhi ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali na vijana kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Mkubwa wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York kuanzia Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa Bahari. 

Akizungumza na wanafunzi na vijana katika mkutano huo leo jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo aliwataka vijana kuwa mstari wa mbele kwa kutoa elimu na kushiriki katika jitihada za kuifadhi mazingira ya bahari pamoja na viumbe waliomo kwa matumizi endelevu. 

Alisema kwa mujibu wa majadiliano katika mkutano uliopita, kasi ya uharibifu wa mazingira ya bahari na viumbe waliomo ni kubwa kiasi ambacho inatishia baadhi ya viumbe kutoweka kabisa kama si kuadimika katika vizazi vya baadaye. 

Alisema taka aina ya nailoni ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikitupwa baharini na kwenye fukwe zinatishia viumbe waliomo baharini na huwenda zikawa na madhara makubwa kwa binadamu hapo baadaye kama jitihada za makusudi hazita chukuliwa. Aliwataka vijana kuwa mabalozi katika kutoa elimu juu ya umuhimu wa kusafisha fukwe na kufanya uvuvi mzuri kwa wavuvi ili kulinda mazalia ya samaki na viumbe wengine majini kwa manufaa ya baadaye. 

Aliongeza kuwa kuna kila sababu ya kuhifadhi mazingira ya bahari kutokana na umuhimu wake kwa maisha ya binadamu. "...Tunapata chakula kutoka baharini (samaki), tunanufaika kwa shughuli mbalimbali kama utalii, ajira katika uvuvi na kazi zingine, biashara, usafiri wa watu na mizigo na shughuli anuai zimekuwa na manufaa makubwa hivyo kuna kila haja ya kila mmoja kuchangia katika kulinda uharibifu wa bahari na mazingira yake," alisema Bi. Stella Vuzo na kuwataka vijana kujitolea mmoja mmoja na katika kusafisha fukwe zetu.

Aidha katika mkutano wa 'The Ocean Conference, United Nations' takribani makubaliano ya ahadi 700 zimetolewa kwa nchi mbalimbali washiriki katika mkutano huo wakiahidi kulinda na kutunza mazingira ya bahari pamoja na viumbe vyake ili visije kutoweka na kutishia manufaa lukuki yatokanayo na uwepo wa bahari na mazingira yake. 

Aliongeza kuwa wameamua kuwapa elimu zaidi vijana kwa kuwa asilimia kubwa ya Watanzania ni vijana hivyo wakiwa na elimu ya kutunza na kuhifadhi fukwe watakuwa mabalozi wazuri wa mapambano hayo ya kulinda mazingira ya bahari. Hata hivyo, Ofisa huyo wa UNIC aliyakaribisha makundi mbalimbali ya vijana kutembelea ofisi za UNIC, Tanzania kujua shughuli mbalimbali wanazozifanya na kuungana katika kampeni anuai zenye manufaa kwa jamii nzima. Baadhi ya wanafunzi wakichangia hoja kwenye mkutano huo ulioandaliwa na UNIC, Tanzania kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Mmoja wa waratibu wa mkutano huo (kushoto), ofisa kutoka Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), akizungumza jambo na wanafunzi na vijana walioshiriki mkutano huo. Baadhi ya wanafunzi wakichangia hoja kwenye mkutano huo ulioandaliwa na UNIC, Tanzania kuzungumzia masuala mbalimbali yaliojiri katika mkutano wa Kimataifa (The Ocean Conference, United Nations) uliofanyika jijini, New York Juni 5-9, 2017 na kukutanisha nchi na wadau anuai wa bahari duniani. Picha ya pamoja ya washiriki katika mkutano huo pamoja na baadhi ya maofisa wa UNIC, Tanzania.

No comments: