Advertisements

Saturday, December 16, 2017

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT JUMA MALEWA AWAAGA MAAFISA MAGEREZA TOKA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WALIOKUWA WAKISHIRIKI MAZOEZI YA ULINZI WA AMANI JIJINI DAR

Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa(kushoto) akiteta jambo na Maafisa wa Magereza/Taasisi za Urekebishaji toka nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika hafla fupi ya kuwaaga iliyofanyika Desemba 15, 2017 katika Ukumbi wa Magereza – Recreation, Ukonga Jijini Dares salaam. Maafisa hao walikuwa hapa nchini kushiriki mazoezi ya Kijeshi ya pamoja kuhusu ulinzi wa amani yaliyohusisha nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) yaliyoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ).Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Charles Novart ambaye pia alikuwa mshiriki kutoka Jeshi la Magereza Tanzania katika mazoezi ya Kijeshi ya pamoja kuhusu ulinzi wa amani akitoa utambulisho kwa Maafisa wa Magereza/Taasisi za Urekebishaji toka nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika hafla fupi ya kuwaaga iliyofanyika Desemba 15, 2017 katika Ukumbi wa Magereza – Recreation, Ukonga Jijini Dares salaam.
Kamishna Msaidizi wa Magereza toka nchini Uganda ambaye pia ni Msemaji wa Jeshi hilo Baine Frank akijitambulisha mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa(hayupo pichani) kwenye hafla fupi ya kuwaaga iliyofanyika katika Ukumbi wa Magereza – Recreation, Ukonga Jijini Dares salaam.
Naibu Kamishna Mwandamizi wa Jeshi la Magereza toka nchini Kenya James Kodieny(kushoto) akiteta jambo na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa(kulia) kama inavyoonekana katika picha katika hafla fupi ya kuwaaga iliyofanyika Desemba 15, 2017 katika Bwalo la Magereza – Recreation, Ukonga Jijini Dares salaam.
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini walioshiriki hafla hiyo ya kuwaaga Maafisa wa Magereza/Taasisi za Urekebishaji toka nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki waliokuwa hapa nchini kushiriki mazoezi ya Kijeshi ya pamoja kuhusu ulinzi wa amani.

Bendi ya Magereza maarufu kwa jina la “MKOTE NGOMA” ikitumbuiza katika hafla hiyo ya kuwaaga Maafisa hao.(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments: