Advertisements

Thursday, December 14, 2017

Video: Msikilize Mbunge wa CHADEMA aliyejiuzuli Ubunge akieleza sababu za Kujiuzulu

Mbunge wa Jimbo la Siha, Mkoani Kilimanjaro kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk. Godwin Oloyce Mollel, aliyetangaza kujivua uanachama wa chama chake na kujiuzulu ubunge amewashukuru wananchi wake wa Siha kwa ushirikiano mkubwa waliompa wakati akiwa madarakani.

Godwin Mollel amejiuzulu nafasi yake ya Ubunge pamoja na kujivua uanachama wa CHADEMA huku akiomba wanachama wa Chama cha Mapinduzi kumpokea na kusema kuwa sababu kubwa iliyomfanya ahame ni kutokana na kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais John Pombe Magufuli katika kupigania rasilimali za nchi.
Bofya hapa kutazama video ya Godwin Mollel akieleza sababu zaidi

No comments: