Advertisements

Sunday, February 18, 2018

Rise Charity wadumisha upendo kwa kuwatembelea Watoto yatima

Katika kusambaza upendo kwa jamii  ya Tanzania ,Shirika lisilo la kiserikali la Rise Charry limeadhimisha kilele cha msimu wa wapendanao kwa kutoa msaada katika kituo cha  sixten Anderson Orphanage Center   kilichopo mkoani pwani, wilaya ya kibaha ikiwa ni miongoni mwa shughuli zinazofanywa na shirika hilo

Maadhimisho hayo ambayo yamehusisha marafiki na wananchi mbalimbali ambao ni watu wa karibu Rise charity pamoja na watoto wa sixten Anderson Orphanage Center yamefanyika katika uwancha wa kituo hicho kwa kusheherekea kwapamoja
Watoto waishio katika kituo cha sixten Anderson Orphanage Center wakipata chakula 
Viongozi mbalimbali wa Rise Charity, Wadau pamoja na watoto wa sixten Anderson Orphanage Center wakiwa katika picha ya pamoja 
Viongozi wa Rise Charity Kulia Mkurugenzi Mtendaji Mr Innocent Horomo, kushoto katibu wa Rise Charity Mr Atley Kayuni na watoto wa sixten Anderson Orphanage Center

No comments: