Advertisements

Wednesday, May 16, 2018

Kondakta Atiwa mbaroni kwa kukutwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia  kondakta wa kampuni  moja ya mabasi yanayofanya safari kati ya Dar es Salaam na Mbeya,baada ya kumkuta na vipodozi vilivyopigwa marufuku.

Mtuhumiwa huyo mkazi wa Kitunda jijini Dar es Salaam alikutwa akiwa amehifadhi vipodozi hivyo katika mifuko miwili ya plasitiki na kwenye boksi.

Akizungumza leo Jumatano Mei 16, 2018 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa baada ya polisi kusimamisha basi na kulifanyia upekuzi.

Amesema tukio hilo limetokea Mei 15, 2018  saa mbili usiku huko maeneo ya Melela Barabara Kuu ya Iringa-Morogoro.

Matei amesema mtuhumiwa alikutwa na vipodozi katoni 56 vya aina tofauti na kwamba vipodozi hivyo vimepigwa marufuku kuingizwa nchini.

Alivitaja vipondozi hiyo kuwa ni Extra Claire tube katoni 23,Lemon Vert Cream katoni 12, perfect white cream  6, betason 4, carolite 3, beiaton 2, extra cream1, sivop cream 1, dyna Claire 1, lemonvet cream 1, princes tube cream 1, epiderm cream 1, exoplus boksi 1, actilua lotion dazen 11, demon Claire pakti 3, oranvet jelly pakti 3 na Claire for men 11


Katika tukio lingine kamanda Matei amesema polisi wanamshikilia  mkazi wa Kikwalaza tarafa ya Mikumi wilayani Kilosa kwa tuhuma za kukutwa na meno ya tembo yenye uzito wa kilogramu 10 zenye thamani ya Sh34 milioni , akiwa amezipakia kwenye baiskeli.

Kamanda Matei amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 15, 2018 na polisi wakishilikiana na maofisa wanyamapori.

Amesema alikutwa akiwa amepakia meno hayo katika baiskeli.

No comments: