Advertisements

Friday, August 10, 2018

RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA AIPONGEZA MAGEREZA KWA UTENGENEZAJI WA THAMANI NZURI NA BIDHAA BORA ZA NGOZI.

Rais Mstaafu wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin William Mkapa akiweka saini kwenye kitabu cha wageni mara tu alipoingia kwenye banda la Magereza kwenye maonesho ya Nane nane yaliyofanyika Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Meneja masoko wa Jeshi la Magereza, Mrakibu Msaidizi Yunge Saganda(tisheti ya Njano na kofia) akitoa maelezo ya namna bidhaa za ngozi zinavyozalishwa kama moja ya shughuli za urekebishaji wa wafungwa katika Gereza Karanga. Mkono wa kulia wa Yunge ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ndg. Antony Mtaka na nyuma ya Mh. Rais Mstaafu ni Katibu Mkuu wa CCM Dk. Bashiru Ally.
Rais Mstaafu Benjamin Mkapa akipata maelezo toka kwa Mrakibu Msaidizi Yunge ya bidhaa zinazotengenezwa kwa kutumia mazao yanayolimwa na Magereza kama vile mchikichi na pamba ambayo hutoa mafuta na husaidia katika utengenezaji wa sabuni.
Mrakibu Msaidizi Yunge Saganda(tisheti ya Njano na kofia) akitoa maelezo kwa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa jinsi bidhaa za nafaka zinazolimwa na wafungwa chini ya uangalizi wa Askari Magereza kama njia ya urekebishaji kwa vitendo zinavyopatikana katika Magereza mbalimbali nchini.
Rais Mstaafu Benjamin Mkapa akiangalia meza ya chai(coffee table) iliyotengenezwa kisanii na kunakshiwa vizuri na wafungwa toka Gereza Uyui Tabora kama moja ya njia za urekebishaji wa wafungwa Magerezani.Kushoto kwa Mh. Rais Mkapa, ni Mama Anna Mkapa ambaye aliaambatana na Mh. Rais.

No comments: